TANZANIA GOSPEL TEAM

Tanzania Gospel Team ni timu ya mpira wa miguu (football) na mpira wa mikono (netball). Timu hii iko nchini Tanzania mkoa wa Dar es Salaam wilaya ya Kinondoni, Sinza Afrikasana.

Timu imejumuhisha wachezaji kutoka makanisa mbalimbali ya Kikristo na hasa waimbaji, maproduza na watangazji wa radio za kikristo.

Lengo la kuanzisha timu hizi ni kumtangaza Kristo kwa njia ya michezo, kuwaunganisha wapendwa wa Bwana kutoka makanisa mbalimbali, kuweka urafiki na undugu, kuijenga miili ya wachezaji kiafya, kuburudisha, kuonyesha mshikamano na ushirikiano kati yetu, kujuana na kufahamiana.

Tangia timu ianze januari 2012 kumekuwa na maendeleo mazuri na watu wengi wamekuwa wakifika katika viwanja vyetu vya mazoezi vilivyooko Sinza Afrikasana katika shule ya Kentoni.  Mungu ametuwezesha kucheza na timu mbalimbali kama vile Dar City FC, Walabata, Pasi Mia, na zingine nyingi.

Tunaomba sana maombi yako ili tuweze kuwa na mafanikio kwa kucheza na timu kubwa kama Manchester, Arsenal, Liverpool, Yanga, Simba n.k

Tunaamini kwa Mungu kila kitu kinawezekana.  

Saturday, March 24, 2012



TANZANIA GOSPEL TEAM YATOKA UWANJANI VICHWA CHINI BAADA YA KUFUNGWA BAO 4-2 NA TIMU YA KOTA FC
Siku ya Jumamosi 25 Machi 2012 katika viwanja vya shule ya Kenton Sinza Mori, timu Kota FC waliwapiga bao 4-2 timu ya Tanzania Gospel bila ya huruma. 

Waliofungua milango ya mabo ni timu ya Kota FC ambayo ilitupia bao la kwanza katika kipindi cha kwanza dakika za mwanzo, na bao la pili lilipatikana katika kipindi hicho hicho. Tanzania Gospel waliamua kushambulia na kujipatia bao la kwanza katika kipindi cha kwanza na baadae kujipatia bao la pili kipindi cha pili. 

Mpaka mpira unaisha Kota FC walitoka na ushindi.....

Washindi KOTA FC 

Timu ya Tazania Gospel 
 Timu ya Kota FC iliyovali uzi wa njano
Mmmoja wa waratibu wa timu ya Tanzania Gospel Team kulia, George Mpela akionge na mchezaji wa TBC1 kuhusiana na mpambano wa leo
 Refalii akiwa na ma-captain wa timu
 Mwimbaji Datsun
 Tanzania Gospel Team wakifanya mazoezi kabla ya mechi
 Wachezaji na mashabiki wakiwa nje ya uwanja
 Goalkeeper  wa Tanzania Gospel
 Kota FC wakiwamsiliza mwalimu wao aliyevalia nyekundi kipindi cha kwanza
Mchezaji wa Kota FC akisaidiwa baada ya kuumizwa

Blogger  Papa Samsasal akiwacheki wachezaji
 Kazi inasonga
 Mabloga, kuanzia kulia Victor(www.hosannainc.blogspot.com), uncle Jimmy (www.unclejimmytemu.blogspot.com), Samsasali (www.samsasali.blogspot.com)



Wednesday, March 21, 2012

TUJIKUMBUSHE: SIKU YA KWANZA TANZANIA GOSPEL TIMU KUANZA MAZOEZI KATIKA VIWANJA VYA SHULE YA KENTON SINZA

Watangazaji wa Praise Power, Uncle Jimmy (kulia) na Deogras Pius (DP)

Kulia ni Meneja wa Praise Power Radio na Kiongozi wa Disciplie katika timu, George Mpela, akifuatiwa na Mtangzaji wa Channel Ten, Boniface Magupa, Mdau wa TGT na kushoto ni mzee wa mablogu na ni Creative Director wa kampuni ya Rumafrica and Africhina, Rulea Sanga

Mtangazaji wa Channel Ten Bony Magupa (kulia) akiwa na Mzee mzima Big-Mtangazaji wa Praise Power, George Mpella..wakitroti....

Saturday, March 17, 2012

GOSPEL TEAM YAITWANGA VIBAYA TIMU YA DAR CITY FC BAO 1-0 SIKU YA IJUMAA
Timu ya Tanzania Gospel iliondoka na ushindi wa bao moja ambalo lilipatika katika kipindi cha kwanza katika uwanja ya shule ya Kenton Sinza. Dar City hawakuamini kipigo walichokipokea kutoka kwa watumishi wa Mungu.
 
 Timu ya Tanzania Gospel

Timu ya Dar City FC 
 Goalkeeper wa Dar City FC haamini kilichopata baada ya mechi kuisha
 Kufungwa kunauma..angalia huyu mchezaji wa Dar City FC baada ya kipigo
 Goalkeeper wa Tanzania Gospel Team, Silas Mbise (wa pili kulia) akitafakari jinsi ya kuudaka mpira wa kona
Mambo yanasonga uwanjani 

Mratibu wa Gospel Tean, Erick Brighton (kulia) hakukosa

Wednesday, March 14, 2012

GOSPEL TEAM YAITWANGA VIBAYA TIMU YA PASI MIA BAO 4-2 KATIKA VIWANJA VYA SHULE YA KENTON SINZA AFRIKASANA-DAR LEO (Jumatano 14 Mach 2012)

Timu ya Gospel ilionekana kuchanganganyikiwa dakika za mwanzo katika kipindi cha kwanza ambapo walipigwa bao mbili kama wamesimama, na baada ya hapo mkono wa Mungu ukaingilia kati kwa watoto wake wa Gospel Team kwa kuwaliza mabao 4-2 . Mchezaji Ayubu wa Gospel Team alionekana kuwaburudisha sana wapenzi wa Gospel team baada ya kuingia kwa kumpokea Anani katika kipindi cha kwanza, alipopiga bao la kwanza, ambalo liliwapa nguvu wachezaji wa Gospel..

Tunaweza kusema Ayubu alifungua milango kwa Gospel Team. Wafungaji wengine ni Masele aliyefunga bao la pili, Mtangazaji wa Chanel Ten, Boniface Magupa alipiga bao la tatu na Francis kijana machachali sana alipiga bao la 4.

Mbali na uchezaji kulitokea vurugu kali kati ya wachezaji wa Pasi Mia na refarii, ambapo walimlalamikia kuwa anapendelea. Kutokana na vurugu hizo kuzidi Victor Aron alimuomba Anania kumsaidia Refarii huyo, lakini hakuwezekana kwa Anania kuwa refarii kwasababu alikuwa mchezaji na kubadilishana na Ayubu kipindi cha kwanza. Maoni yakapendekezwa kwa mfanyabiashara maarufu sana jiji Dar es Salaam, Zizzou kuwa refarii.

Mechi ikatulia na ikawa ya kufurahisha sana kutokana na refarii huyo kuwanyamazisha wachezaji na kuwaonya kuwa atayecheza fujo atatolewa nje ya uwanja.

Timu zikiwa fiti kuanza mpambano


Timu ya Tanzania Gospel Team ikiwa na kocha wao, Felix Msele (kulia)


Kazi imeanza


 Wachezaji walioko bench wakijiandaa kuingia, Geoge Mpella (kulia) akiwa ametulia

 Mchezaji wa Gospel Team na mtangzaji wa Praise Power Radio, Kisaka akiongea na blogger Rulea Sanga kuhusiana na ushindi 
 Blogger, Rulea Sanga aliyevalia Tshirt yenye msalaba akimsikiliza captain wa timu ya Gospel timu Yona Jakobo

 Kocha wa Gospel Team, Felix Masele (kulia) na kaptain wa timu hiyo, Yona Jakobo wakiteta jambo
 Mfungaji wa goli la kwanza wa Gospel Team, Ayubu akiwa ameshika kiuno akijiandaa kuingia uwanjani