TANZANIA GOSPEL TEAM

Tanzania Gospel Team ni timu ya mpira wa miguu (football) na mpira wa mikono (netball). Timu hii iko nchini Tanzania mkoa wa Dar es Salaam wilaya ya Kinondoni, Sinza Afrikasana.

Timu imejumuhisha wachezaji kutoka makanisa mbalimbali ya Kikristo na hasa waimbaji, maproduza na watangazji wa radio za kikristo.

Lengo la kuanzisha timu hizi ni kumtangaza Kristo kwa njia ya michezo, kuwaunganisha wapendwa wa Bwana kutoka makanisa mbalimbali, kuweka urafiki na undugu, kuijenga miili ya wachezaji kiafya, kuburudisha, kuonyesha mshikamano na ushirikiano kati yetu, kujuana na kufahamiana.

Tangia timu ianze januari 2012 kumekuwa na maendeleo mazuri na watu wengi wamekuwa wakifika katika viwanja vyetu vya mazoezi vilivyooko Sinza Afrikasana katika shule ya Kentoni.  Mungu ametuwezesha kucheza na timu mbalimbali kama vile Dar City FC, Walabata, Pasi Mia, na zingine nyingi.

Tunaomba sana maombi yako ili tuweze kuwa na mafanikio kwa kucheza na timu kubwa kama Manchester, Arsenal, Liverpool, Yanga, Simba n.k

Tunaamini kwa Mungu kila kitu kinawezekana.  

Monday, July 9, 2012

SHETANI ANAYOSUMBUA WANADAMU

Mwandishi: Rulea Sanga

Ndugu zangu nyakati hizi ni za kumtafuta Mungu na kufanya kazi ya Mungu. Ulimwengu umeharibika, taarifa za kutisha na za kukatishana tamaa zimezidi. Watu wanaishi maisha ya hofu, hawana amani ndani ya maisha yao. Ndoto za ajabu zimewatala, zinawafanya waishi maisha ya wasiwasi. Binadamu wamekuwa wanyama, hawana huruma na wanapenda kuona wenzao wanateseka.

Wengine hawapendi hata kuona mwenzao anafanikiwa, wako tayari kutumia njia zozote kuhakikisha mambo yako yanaharibika. Imani za kishirikina zimetawala, watu wanalogana, watu wako tayari kupoteza maisha ya wenzao ili mradi mambo yao yanasonga mbele. Ukipita mitaani utakutana na vichaa wanahangaika na wengine wako uchi- hakuna wa kuwasitiri. Watoto na watu wazima wanachukuliwa misukule, wanafanyiwa mambo ya ajabu huko misituni na wachawi, vyakula vyao ni vya ajabu. 
 
Kuna baadhi ya watu wamezuiliwa milango yao ya mafanikio na ndugu zao au jamaa zao. Kila unapojitahidi kufanya jambo fualni, halifanikiwi. Wengine wanajitahidi kusoma kwa bidii, lakini wanapokuja kufanya mitahini ya mwisho wanafeli, ila ukiangalia maendeleo yao kabla ya mitihani yalikuwa mazuri sana. Kuna wengine wamelogwa na kusemewa maneno mabaya na wabaya ya kuwa kila jambo utakalofanya hutafanikwa, nah ii imetawala sana katika kipindi hiki.

Wachawi wanawaloga watu na kuwatupia majini na kuwasemea maneno mabaya. Utaona msichana ni mrembo sana na amefanikiwa kimaisha lakini hapati mtu wa kumuoa. Wasichana kama hawa wanafikia hatua hata ya kuwa wabaya katika jamii na kuona kama wametengwa na ulimwengu. Wanatamani kufanya vitendo viovu na kudiriki kuingia katika ushiriana ili wapate waume. Na hili sio tu kwa wasichana bali hata kwa wanaume ambao nao hujiingiza katika mambo maovu ya ushoga, ushirikina, ulevi, utekaji, uchawi, wizi na mambo mengine kama hayo.

Barabarani lusambazwa nuksi za kila aina, ajali zimetawala. Wachawi wanaweka mambo yao ya ajabu katika barabara ili kusababisha ajali, na ajali inapotokea wao hufurahia kwani kwao damu ma myama ya watu ndio chakula chao kikuu na ndicho kinachowasaidia kufanikiwa mambo yao. Hili ni ja,bo la kusikitisha sana na linaumiza sana hasa pale unaposikia ndugu yako amepoteza maisha kwa jajali mbaya.

Vita ndani ya familia zimetawala sana katika ulimwengu huu, kuna baadhi ya familia hazielewani, utaona mama na mototo wake wanatukana na kushikiana visu ili wauane. Shetani ametawala katika familia zetu. Hapendi kuona wewe unaelewana na ndugu yako. Anajitahidi kutumia mbinu zake kuhakikisha hakuna amani katika familia yako. Cha kushangaza utaona pengine katika familia kuna wengine wamefanikiwa kiuchumi na nimatajiri sana, lakini ndani ya hiyo familia kuna maskini wakutupwa na hakuna wakuwasaidia. Shetani mara nyingine anaweza kukuzuia wewe kutokuwa na moyo wa kusaidia jamii yako, au anaweza kuzuia wewe maskini kuonekana hufai kwa yule ndugu yako aliyefanikiwa

Wasomi wengi wamesoma lakini wanakosa kazi, kila wakienda kuomba kazi hawafanikiwi. Kuna baadhi ya ofisi ukipeleka vyeti vyako na wakiona wewe umesoma sana wanakataa kukupa kazi eti kwasababu umesoma sana na hawataweza kukulipa mshahara kulingana na elimu yako. Shetani ni majanja sana na ni mjinga, huwapa wajiri kipofu cha kufikiri na kuwadanganya kwa kuwapa “statement” ambayo ni ya kipimbavu ya kuwafukuza wasomi wazuri ambao wangeweza kuinua kampuni. Baadhi ya wasomi wengine hawaangalii sana kiwango cha msharaha ila wanachotaka na “experience” tu ya kazi.

Shetani hana huruma kwa wanadamu, kuna baadhi ya watu wamelogwa kuwafanya mazezeta, wengine chakula chao ni mikaa ya moto, barafu, kinyesi, mikojo, michanga, kucha, na vitu ambavyo mwanadamu hawezi kuvila. Furaha yake ni kuona unateseka na hufanikiwi kwa lolote. 
 
Ombi langu kwako unayeteseka, jaribu kuwa karibu sana na Mungu kwa kufanya mapenzi yake mema. Pia kuwa na imani kwa kila jambo unaloomba kwa Mungu kuwa linaenda kufanyika. Kumkemea shetani kuwe ni moja ya kazi yako ya kila siku. Maombi yasipungue katika kinywa chako. Na unapoomba umaanishe na usiweke kama ratiba fulani. Maombi yako yawe silaha katika kupambana na adui shetani. Tafuta watu waliokoka kabisa na anza kushirikiana nao katika kusoma biblia na kuijadili ili kuwa na ufahamu wa kutosha kuhusiana na Mungu. Epukana na wanaokukatisha tamaa kuhusu Mungu. Ukiwa na Mungu utapambana na watu wengi ambayo watakukatisha tamaa, na huyo ni shetani kwani shetani mara zingine anatumia watu au rafiki au ndugu zako na kukuletea habari mbaya kuhusu Mungu.
 
Mungu wangu akubariki







No comments:

Post a Comment