TANZANIA GOSPEL TEAM

Tanzania Gospel Team ni timu ya mpira wa miguu (football) na mpira wa mikono (netball). Timu hii iko nchini Tanzania mkoa wa Dar es Salaam wilaya ya Kinondoni, Sinza Afrikasana.

Timu imejumuhisha wachezaji kutoka makanisa mbalimbali ya Kikristo na hasa waimbaji, maproduza na watangazji wa radio za kikristo.

Lengo la kuanzisha timu hizi ni kumtangaza Kristo kwa njia ya michezo, kuwaunganisha wapendwa wa Bwana kutoka makanisa mbalimbali, kuweka urafiki na undugu, kuijenga miili ya wachezaji kiafya, kuburudisha, kuonyesha mshikamano na ushirikiano kati yetu, kujuana na kufahamiana.

Tangia timu ianze januari 2012 kumekuwa na maendeleo mazuri na watu wengi wamekuwa wakifika katika viwanja vyetu vya mazoezi vilivyooko Sinza Afrikasana katika shule ya Kentoni.  Mungu ametuwezesha kucheza na timu mbalimbali kama vile Dar City FC, Walabata, Pasi Mia, na zingine nyingi.

Tunaomba sana maombi yako ili tuweze kuwa na mafanikio kwa kucheza na timu kubwa kama Manchester, Arsenal, Liverpool, Yanga, Simba n.k

Tunaamini kwa Mungu kila kitu kinawezekana.  

Sunday, May 20, 2012


FADHAGET SANITARIUM CLINIC CD KUPATIKA SASA-Dr. Fadhili Emily
Dokta Fadhili amesema sasa unaweza kupata mafundisho kuhusiana na huduma za tiba zinazotolewa na Sanitarium Clinic iliyoko Mbezi Beach Tangi Bovu, Tandika Majaribio-Dar es Salaam Tanzania

Amewaomba watu wote kununua CD hii ili uweze kujifunza ni jinsi gani unaweza ukatibiwa magonjwa sugu kwa njia ya mimea na matunda.

Kama ungependa kujua zaidi jinsi ya kupata hizi CD, tafadhali wasiliana nasi kwa mawasiliano yaliyopo katika CD hapo chini:-




CD case imetengenezwa na Rulea Sanga +255 715 85 15 23 | rumatz2011@yahoo.com | www.rumaafrica.blogspot.com

No comments:

Post a Comment